Friday, August 23, 2019

Kampuni ya Nebrix Ltd ni Mzabuni wa Kuigwa katika Sekta ya Elimu Misungwi"


  1. Misungwi; Afisa Masoko wa Kampuni ya Nebrix Ltd, Mwanza, Ayubu Robert  Ng”hwelo amekabidhi msaada wa Vitabu  50 (masomo mbalimbali), Tufe 1, Dustbin 5 za kuhifadhia taka laini, Heart Model 1, Charts 20, First Aid Kit 1, na Skeleton Model 1 kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya (w) Misungwi Bw, Kisena Mabuba kwa lengo la kuvipeleka katika shule za Sekondari zilizoko Misungwi ili kuleta ufanisi katika tendo zima la Ufundishaji na Ujifunzaji. Vifaa vilivyotolewa vina thamani ya Tsh. 4,300,000/= (milioni nne na laki tatu tu) 

    Akipokea vifaa hivyo Mkurugenzi wa Halmashauri ya (w) Misungwi Ndg, Kisena Mabuba ameishukuru kampuni hiyo kwa kuona ni vyema kusaidia shule za sekondari kwa vifaa mbalimbali walivyotoa, hii inaonyesha wanajali sana elimu kwa maana wameweza kutumia faida waliyoipata kusaidia kuinua elimu katika wilaya yetu ya Misungwi. Hii ni moja ya kujivunia wazabuni ikiwa wanarejesha faida katika shughuli za maendeleo (returns) na kwa kufanya hivyo tutakuwa wazalendo kwa taifa letu.

    Kitendo hiki cha kujitoa kusaidia kuinua elimu  kwa vifaa vilivyotolewa kimemfurahisha Bi, Dianah Kuboja Afisa Elimu Sekondari wilaya ya Misungwi, na amesema vifaa vilivyotolewa vitapelekwa katika  shule mbili za sekondari ambazo zimeanza hivi karibuni ili kukabiliana na upungufu uliopo ambazo ni shule ya sekondari Mamaye na J. Magufuli.


    Shukurani za pekee kwa Kampuni ya Nebrix Ltd kutambua umuhimu wa Elimu, na kuweza kutoa mchango wao ili kuinua kiwango cha ufaulu katika sekta ya elimu ngazi ya sekondari Misungwi.

    0

    Ongeza maoni



    Inapakia

    Thursday, August 8, 2019

    "Kujengwa kwa Soko la Dhahabu Shilalo ni Chachu na Uhakika wa Soko kwa Wachimbaji wa Dhahabu"


    Misungwi: Mkuu wa wilaya ya Misungwi Mh. Juma Sweda akikagua mojawapo ya soko la madini ya Dhahabu linalojengwa Misungwi katika eneo la Shilalo ambapo kuna shughuli za uchimbaji mdogo hzinazoendelea kwa wachimbaji wadogo kuchimba Dhahabu na kuuza ili kujipatia fedha ya kujikimu katika maisha yao ya kila siku. Mkuu wa wilaya amewaomba wachimbaji hao kutumia soko hilo wakati wa kuuza Dhahabu yao ili kujipatia kipato na kuifanya serikali iweze kukuza uchumi wake kutokana na Dhahabu inayopatikana katika maeneo yetu, kutokana na kodi itakayopatikana kwa mujibu wa sheria za madini. Uanzishwaji wa masoko haya ni kuepusha uuzwaji holela wa Dhahabu unaoikosesha serikali kipato. Wachimbaji wa madini wadogo katika eneo la Shilalo, tutumieni soko hili kwa kuuza rasilimali yetu adimu ya Dhahabu ili kuinua uchumi wa Shilalo, wilaya yetu ya Misungwi na taifa letu kwa ujumla. Mipango na mikakati ya awamu ya tano ni endelevu kwa kuhakikisha inainua uchumi na kipato cha kila mwananchi (Mtanzania) kwa kumjengea mazingira bora ya uzalishaji Mali.


    Pichani; ni baadhi ya wachimbaji wadodo katika machimbo ya Dhahabu Shilalo wakiwasikiliza viongozi kwa makini juu ya utumiaji wa masoko ya madini wakati wa kuuza Dhahabu wanayoipata kutokana na shughuli yao ya uchimbaji.

    Pichani hapo juu; ni mojawapo ya mashine ya kusaga mawe ya Dhahabu alimaarufu hujulikana kwa jina la Karasha.

    Pichani; ni sehemu mojawapo inayotumika kwa shughuli ya uoshaji wa Dhahabu baada ya mawe ya Dhahabu kusagwa, alimaarufu hujulikana kama sehemu ya kuchenjulia Dhahabu.




    Monday, July 15, 2019